Yetu Microfinance Bank PLC
YETU MICROFIN
  • Home
  • About us
    • Vision and Mission
  • Bank Services
    • Bank Accounts
    • Loans Services
    • ATM Services
    • Yetu Insurance
    • Mobile banking
  • Resource Center
    • Financial reports
    • Green House Training
    • Publications
    • Prospectus
    • Download Prospectus
  • Contact us
    • Head office
    • Our Branches
  • Careers
September 1 2016

Mkutano wa kwanza wa wanahisa

administrator Uncategorized

TAARIFA INATOLEWA KWAMBA, Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Wanahisa wa Yetu Microfinance Bank Plc utafanyika siku ya Jumamosi tarehe 24 Septemba, 2016 katika Ukumbi wa Msimbazi Centre, Dar es Salaam kuanzia saa nne asubuhi.

Agenda

  1. Kuridhia Agenda za Mkutano.
  2. Kuchagua na kuthibitisha Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi.
  3. Mengineyo

Maelezo

  1. Mwanahisa atakayehudhuria Mkutano Mkuu atatakiwa kujigharamia mwenyewe na aje na Hati ya Hisa iliyotolewa na Soko la Hisa la Dar es Salaam pamoja na kitambulisho chake,kadi ya kupiga kuira au hati ya kusafiria au kitambulisho cha kazi. Fomu ya mwakilishi mbadala(proxy form) itapatikana  ofisi za YETU,makao makuu zilizopo Jengo la Mkunazini, ghorofa ya 2,mtaa wa Kiungani-Kidongo Chekundu  na matawi yote  na ofisi za madalali wa Soko la Hisa Dar es Salaam kuanzia tarehe 9 Septemba,2016.
  2. Mwanahisa anayestahili kuhudhuria na kupiga kura lakini akashindwa kuhudhuria kikao,anaweza kuwasilisha Jina la mbadala wake(proxy) kwa Katibu wa Bodi  katika  ofisi za YETU makao makuu zilizopo jengo la Mkunazini, ghorofa ya 2,mtaa wa Kiungani-Kidongo chekundu au kwenye kikao. Kwa makampuni, fomu inapaswa kuwa katika lakiri ya kampuni mwanahisa.
  3. Ili kujua wanahisa wanaostahili kupiga kura ,Rejesta ya Wanahisa itafungwa Jumatano tarehe 21 Septemba,2016.

 

TAARIFA YA SEMINA KWA WANAHISA

Taarifa inatolewa kwamba kutakuwa na semina kwa Wanahisa itakayolenga kutoa elimu kuhusu “Jinsi Wawekezaji Wanavyoweza Kutumia Fursa za Uwekezaji Katika Soko la Hisa” Semina hiyo itafanyika Ijumaa, tarehe 23 Septemba,2016 katika ukumbi wa Msimbazi Centre, kuanzia saa 3.00 asubuhi.

 

KWA IDHINI YA BODI

 

Joyceline Kobero

Katibu wa Benki

Septemba , 2016             

Vacancy- Cashier 4 Posts Vacancy- Risk management and compliance officer

Related Posts

financial-statements-28845002

Uncategorized

Financial Statements December 2017

shares

News, Uncategorized

FOMU NA MAELEKEZO YA GAWIO LA HISA

DIVIDENDS

Uncategorized

DIVIDEND ANNOUNCEMENT

Siku ya leo

June 2023
M T W T F S S
 1234
567891011
12131415161718
19202122232425
2627282930  
« Feb    
Yetu Microfinance Bank PLC
  • Home
  • About Us
  • Our products
    • Loans Services
    • Savings
    • Mobile banking
    • Housing Loans
    • ATM Services
    • POS devices
  • Resource center
    • Green House Training
    • Partners/Alliances/Sponsors
    • Publications
    • Financial reports
  • Media centre
    • Photo Gallery
  • IPO
    • IPO EXTENSION
    • Special dates
    • Executive summary
    • Full prospectus
  • Contact us
    • Head office
    • Our Branches
    • Our financial services centres
    • Complaint resolution unit
  • Careers
    • Prospectus
  • Yetu Insurance
  • Bank Accounts
© Yetu Microfinance Bank PLC 2023
Proudly powered by Lematrix Tanzania